CASFETA ni jumuiya ya Wanafunzi mabalozi wa Kristo Tanzania iliyoanzishwa mwaka 1992. Wazo lake lilianzia kwa
viongozi wa idara ya vijana wa TAG, yaani Christ’s Ambassadors (CAs). Aliyekuwa katibu mkuu wa CAs, Mchungaji Uswege
Mwakisyala alikuwa ndiye mwenyekiti wa kamati ya watu watatu waliotengeneza mwongozo wa kwanza wa CASFETA. Wajumbe
wengine wa kamati hiyo ni Joseph Justine na ndugu Godfrey Mdoe. Lengo lilikuwa ni kupata chombo cha kuhudumia vijana
waliookoka wa kipentekoste walioko mashuleni na vyuoni. Jina (CASFETA) yaani Christ’s Ambassadors Student Fellowship
Tanzania lilibuniwa na Mchungaji ambaye sasa ni Askofu Uswege Mwakisyala. Jina hilo lina asili yake ni katika jina la
idara ya Vijana ya kanisa la TAG....
Mwongozo huo alipewa Joseph Justine akiwa
anafanya huduma ya wanafunzi na JUWAKWATA. Viongozi wa kwanza walikuwa kama ifuatavyo; Mwenyekiti alikuwa Doroty Mhando
(Sasa ni Mrs D.Massawe yuko TAG Kinondoni), Katibu alikuwa Emanuel Akili na wajumbe wengine kama Elisha Joseph. Viongozi
hao waliandika barua yao kwa askofu mkuu wa TAG tarehe 9/7/1992 kupitia kwa mkurugenzi mkuu wa CAs.
Askofu mkuu wa wakati huo Mchungaji Ranwel Mwenisongole alijibu kwa barua yake ya tarehe 8/10/1992, kuikubali huduma hiyo
ianzishwe na kusimamiwa na idara ya vijana CAs. Tarehe hiyo hiyo katibu mkuu aliandika barua kwenda wizara ya elimu ili
kuitambulisha rasmi huduma ya wanafunzi.
Joseph Justine aliteuliwa kuwa mratibu mkuu akiwa mhitimu wa chuo cha biblia akifanya huduma chini ya Mchungaji Titus
Mkama wa ilala TAG. Kwa nafasi yake kama mratibu mkuu aliandika barua inayoitambulisha CASFETA kwa taasisi mbalimbali nchini
kuwa ni huduma inayodhaminiwa na kukulewa na kanisa la TAG. Mwaka 1993 mwongozo wa CASFETA wa kwanza ulibadilishwa ili kukidhi
hoja ya kuifanya CASFETA ya wanafunzi wote wa makanisa ya kipentekoste.
Mwaka 1998 Joseph Justine aliasi maongozi ya TAG kisha akateuliwa mkurugenzi mpya wa CASFETA Mch. Mwakisyala kwa barua ya tarehe
16/11/1998 iliyopelekwa wizara ya elimu na kanisa la TAG ikiifahamisha wizara mabadiliko ya Uongozi. Baada ya uasi kutokea TAG
ilimtenga ushirika wa kanisa mwaka 1998. Pamoja na changamoto hizo CASFETA iliendelea chini ya mkurugenzi mkuu Mch. Mwakisyala
mpaka 2008 ikiwa na matawi zaidi ya 500. Mwaka 2008 CASFETA ilipata mkurugenzi mpya Mch. Dk, Huruma Nkone ambaye katika uongozi
wake iliendelea kukua na kuzifikia shule, vyuo na vyuo vikuu vingi hapa nchini Tanzania. Kufikia mwaka 2020 kumekuwa na matawi zaidi
ya elfu mbili mia tisa nchini kote.
Kwa sasa CASFETA inazidi kukua kwa kasi kubwa zaidi ikihudumia wanafunzi mbalimbali kutoka madhehebu ya kipentekoste nchini na kusimamia
makusudi ya uwepo wake kama iliyoainishwa katika website hii. Ili kuendelea kukua katika dhamiri njema ya kuwalea wapentekoste wote mashuleni
na vyuoni, Mwongozo wa CASFETA umeboreshwa sana na mpaka sasa CASFETA inatumia mwongozo wake toleo Rasmi la mwaka 2021.
Kuwa kizazi kinachotembea katika nguvu za Roho Mtakatifu na kuubadilisha ulimwengu kwa Neno la Mungu.
Kuwawezesha wanafunzi kumwabudu Mungu kulingana na imani yao ya kipentekoste.
Kuwafikia wanafunzi wote kwa Injili ya Kristo kimkakati na kuwajenga kiroho kwa njia ya Kuabudu na Ushirika.
CASFETA ni jumuiya ya Wanafunzi mabalozi wa Kristo Tanzania iliyoanzishwa mwaka 1992. Wazo lake lilianzia kwa viongozi wa idara ya vijana wa TAG, yaani Christ’s Ambassadors (CAs).
MKURUGENZI
CASFETA imenisaidia kuongeza kiwango changu cha kufunga na kuomba pamoja na uongozi.
Aliyekua Mwanafunzi
Idara ya Casfeta ilinisaidia kua na ujasiri wa kuhubiri mbele za watu wengi.
Mwanafunzi